Wimbi La Siasa

Kwanini wakaazi wa Uvira hawamtaki Jenerali Olivier Gasita ?

Informações:

Sinopsis

Mji wa Uvira, jimboni Kivu Kusini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa zaidi ya wiki moja, ikiwemo Septemba 08, umeshuhudia maandamano yaliyopangwa na mashirika ya kiraia na wapiganaji wa Wazalendo, kupinga kupinga kuteuliwa kwa Jenerali Olivier Gasita, kuwa Naibu Kamanda wa Kikosi cha jeshi la FARDC, katika eneo hilo kwa madai ya kuwa na ushirikiano na waasi wa AFC/M23 kwa sababu ya kabila lake la Banyamulenge.