Siha Njema

Je unafahamu vipimo vya afya unavyohitaji kupima kabla kufunga ndoa?

Informações:

Sinopsis

Watu wengi wanapokaribia kufunga ndoa,hujukumika kufanya vipimo vya virusi vya HIV .Wengi hufanya kipimo hicho si kwa sababu wanajua umuhimu wake bali ni kwa sababu ya ulazima kabla kufunga harusi haswa za Kikristo. Hata hivyo watalaam wa afya wanasema kuna vipimo tele ambavyo ni muhimu pia na vinahitajika kufanywa kabla ndoa. Mwanasaikolojia Naomi Ngugi  anasema kando na kipimo cha HIV,kuna  kipimo cha Rhesus Factor ambayo kama mtu na mwenzake hana ufahamu ,wanaweza kupata shida ya kuharibika mimba. Kuna pia kipimo cha  Genotype  kubaini uwepo wa ugonjwa kama  Selimundu ,Hepatitis B,  Hepatitis C au homa ya ini,vipimo vya  Magonjwa sugu, Magonjwa ya akili na Vipimo vya uzazi kubaini ubora wa mbegu za kiume na matatizo ya  mirija kuziba upande wa wanawake.   Vipimo hivyo vinaweza kugharimu ndoa iwapo wanandoa hawataweka wazi.