Siha Njema

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 4:00:13
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Makala inayojadili kwa kina masuala ya afya, tiba na kutambua magonjwa mbalimbali bila ya kusahau namna ya kukabiliana nayo. Watalaam walibobea kwenye sekta ya afya watakujuvya na kukuelimisha juu ya umuhimu wa kuwa na afya bora na si bora afya. Pia utawasikiliza kwa maneno yao watu ambao wameathirika na magonjwa mbalimbali na walikumbwa na nini hadi kufika hapo walipo.

Episodios

  • Kukata kiu ya jamii zinazoishi mpaka wa Kenya na Somalia ,waathiriwa wa mgogoro

    25/02/2025 Duración: 08min

    Mamia ya wakaazi wa kaskazini  mashariki mwa Kenya maeneo yanayopakana na Somalia na waathiriwa wakubwa wa mzozo wa Somalia hawajakuwa na maji masafi , hali hiyo ikizidisha mgogoro wa kijamii ndani ya jamii hii ya wafugaji wanaotokea upande wa Kenya na  upande mwingine wa Somalia. Kukabili hali  hii ,kamati ya kimataifa ya msalaba mwekundu , International Committee  of the Red cross ,ICRC , shirika la msalaba mwekundu nchini Kenya ,Kenya Red Cross,KRC katika mkakati wa kuleta amani na ustawi imekuwa ikifanya miradi ya kuwapa wakazi maji .Carol Korir amezuru eneo la Masalani ,kaunti ya Garissa  kilomita chache na msitu wa Boni  ambapo Al shabab wamekuwa wakifanya mashambulizi  na kujificha .

  • Utayari wa ukanda wa Afrika kupambana na magonjwa ya milipuko

    19/02/2025 Duración: 10min

    Katika siku za hivi punde magonjwa ya milipuko imeripotiwa katika mataifa ya Afrika ,ikiwemo Ebola Marburg na Mpox

  • Juhudi za Guinea kumaliza ugonjwa wa Malale mojawapo ya magonjwa yaliyotengwa

    05/02/2025 Duración: 10min

    Guinea itakuwa ni taifa la nane la Afrika kuthibitishwa kuangamiza ugonjwa wa malale Guinea imekuwa ilishiriki katika majaribio ya matibabu ya ugonjwa wa malale ambayo yalifanyiwa utafiti mara ya kwanza nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya CongoTimu ya madaktari kutoka DRC na Guinea walishirikishwa kwenye majaribio hayo na kwenye makala haya tumezungumza na Dkt Chirac Bulanga kutoka DRC

  • Ugonjwa wa Ukoma bado ni changamoto kubwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

    29/01/2025 Duración: 09min

    DRC imeripoti maambukizi ya Ukoma mwisho wa mwaka jana na pia mwaka huu Ukoma ni ugonjwa unaoathiri sana ngozi na unaweza kuharibu baadhi ya viungo kama vile mikono ,miguu na hufanya mtu kutengwa na jamii

página 2 de 2