Gurudumu La Uchumi

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 3:59:19
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Fahamu masuala kadha wa kadha kuhusu uchumi kama vile, namna ya kupambana na umaskini, mfumuko wa bei, kushamiri kwa matumizi ya dola na athari za kuyumba kwa uchumi wa dunia kwa nchi za Afrika. Mada hizi zinafanyiwa utafiti wa kina na zinazungumzwa kwa lugha rahisi inayoeleweka ili kukufanya uelewe na usichoke kusikiliza .

Episodios

  • Miundombinu; changamoto ya upatikanaji wa nishati (umeme) Afrika

    12/03/2025 Duración: 10min

    Wiki hii katika makala ya Gurudumu la Uchumi, tunajadili changamoto za upatikanaji wa nishati ya uhakika barani Afrika, ambapo pamoja na baadhi ya mataifa kuwa na rasilimali za kutosha kuzalisha nishati ya ziada, suala la miundombinu limeendelea kusalia kikwazo, ambapo baadhi ya mataifa yanalazimika kununua nishati toka mataifa jirani.Ali Mkimo, mchambuzi na mtaalamu wa masuala ya Uchumi atakuwa nasi kudadavua hili kwa kina.

  • Athari kwa uchumi wa dunia kutokana na vikwazo vya kibiashara vilivyotangazwa na Marekani

    05/03/2025 Duración: 09min

    Katika makala ya Gurudumu la Uchumi juma tunajadili athari za kibiashara kimataifa kutokana na hatua ya hivi karibuni ya Marekani kutangaza vikwazo vya kikodi kwa mataifa ya Canada, Mexico, India na Uchina ambao ni washirika wake wakubwa kibiashara.Kujadili hili, kwenye line ya simu tunaungana na Profesa Wetengere Kitojo, mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

  • Sehemu ya Pili: Afrika na harakati za kudai mabadiliko kwenye taasisi za kifedha za kimataifa

    26/02/2025 Duración: 09min

    Msikilizaji juma lililopita tulianza kwa kujadili yaliyotokana na mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika, na suala kuu lilikuwa ni je, nchi za Afrika zitafanikiwa kushinikiza mabadiliko katika taasisi za kifedha za kimataifa na kuondokana na mikopo na madeni yasiyostahimilika ?Leo katika makala ya Gurudumu la Uchumi, nakuletea sehemu ya pili ya mjadala huu, nimemualika Ali Mkimo, mtaalamu namchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa nchini Tanzania.

  • Je, Afrika itafanikiwa kushinikiza mabadiliko katika mifumo ya kimataifa ya kifedha

    19/02/2025 Duración: 10min

    Msikilizaji mwishoni mwa wiki iliyopita, viongozi wa Afrika waliokutana mjini Addis Ababa, Ethiopia, walikubaliana kuongeza kasi ya kudai mabadiliko kwa mifmo ya kifedha ya kimataifa, ili kuziwesha kuwa na nafasi katika maamuzi. Afrika inalalamika kutokuwepo usawa, na hivyo kuyaweka mataifa ya Afrika katika hali ya kutegemea mikopo yenye masharti magumu.Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, tunajadili ikiwa azma hii ya viongozi wa Afrika itafanikiwa.

página 2 de 2